Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis * - Translations’ Index


Translation of the meanings Surah: An-Naml   Ayah:

An-Naml

طسٓۚ تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡقُرۡءَانِ وَكِتَابٖ مُّبِينٍ
«Tā Sīn» Yametangulia maelezo kuhusu herufi zilizokatwa na kutengwa katika mwanzo wa sura ya Al-Baqarah. Hizi ni aya za Qur’ani, nazo ni aya za Kitabu kitukufu zenye maana yaliyofunuka wazi zenye ushahidi waziwazi wa kuonyesha elimu zilizomo, hekima na Sheria.
Arabic explanations of the Qur’an:
هُدٗى وَبُشۡرَىٰ لِلۡمُؤۡمِنِينَ
Nazo ni aya zenye kuongoza kwenye njia ya kufuzu duniani na Akhera, na zinatoa bishara ya malipo mazuri kwa Waumini walioziamini na wakaongoka kwa uongofu wake.
Arabic explanations of the Qur’an:
ٱلَّذِينَ يُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَيُؤۡتُونَ ٱلزَّكَوٰةَ وَهُم بِٱلۡأٓخِرَةِ هُمۡ يُوقِنُونَ
Ambao wanasimamisha Swala tano zilizotimia nguzo, zilizokamilika masharti, na wanatekeleza Zaka za lazima kwa wanaostahiki kupewa, na wao wanaamini kwa yakini maisha ya Akhera na yaliyomo ndani yake ya malipo mema na mateso.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ زَيَّنَّا لَهُمۡ أَعۡمَٰلَهُمۡ فَهُمۡ يَعۡمَهُونَ
Hakika ya wale wasioamini nyumba ya Akhera na hawafanyi matendo ya kuwafaa huko, tutawapambia wao matendo yao mabaya wayaone ni mazuri, na wao watakuwa wakizunguka kwenye matendo hayo wakiwa wameduwaa.
Arabic explanations of the Qur’an:
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ لَهُمۡ سُوٓءُ ٱلۡعَذَابِ وَهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ هُمُ ٱلۡأَخۡسَرُونَ
Hao ndio watakaopata adhabu mbaya duniani, kwa kuuawa, kutekwa, kudhalilika na kushindwa. Na wao huko Akhera watakuwa ni wenye hasara kubwa zaidi.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِنَّكَ لَتُلَقَّى ٱلۡقُرۡءَانَ مِن لَّدُنۡ حَكِيمٍ عَلِيمٍ
Na kwa hakika wewe , ewe Mtume, unapewa Qur’ani kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Mwingi wa hekima katika kuumba Kwake na upelekeshaji Wake Ambaye Amekizunguka kila kitu kwa kukijua.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِأَهۡلِهِۦٓ إِنِّيٓ ءَانَسۡتُ نَارٗا سَـَٔاتِيكُم مِّنۡهَا بِخَبَرٍ أَوۡ ءَاتِيكُم بِشِهَابٖ قَبَسٖ لَّعَلَّكُمۡ تَصۡطَلُونَ
Taja habari ya Mūsā aliposema kuwaambia watu wa nyumbani kwake katika safari yake kutoka Madyan kwenda Misri, «Mimi nimeuona moto. Nitawajia kutoka huko na habari ya kutuonyesha njia, au nitawajia na kinga cha moto mupate mvuke wake mjihami na baridi.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَلَمَّا جَآءَهَا نُودِيَ أَنۢ بُورِكَ مَن فِي ٱلنَّارِ وَمَنۡ حَوۡلَهَا وَسُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Mūsā alipoujia moto, Mola wake Alimwita na akampa habari kwamba hapa ni mahali Alipopatakasa Mwenyezi Mungu na Akapabariki na Akapafanya ni mahali pa kusema na Mūsā na kumtumiliza, na kwamba Mwenyezi Mungu Amewabariki waliopo motoni na waliopo pambizoni mwake miongoni mwa Malaika, na kumtakasa Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe, kwa kumuepusha na sifa zisizonasibiana na Yeye,
Arabic explanations of the Qur’an:
يَٰمُوسَىٰٓ إِنَّهُۥٓ أَنَا ٱللَّهُ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ
«Ewe Mūsā! Hakika yangu mimi ni Mwenyezi Mungu ninayestahiki kuabudiwa peke yangu, ni Mshindi Mwenye nguvu wa kuwaadhibu maadui zangu, niliye na hekima katika upelekeshaji wa viumbe vyangu.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَأَلۡقِ عَصَاكَۚ فَلَمَّا رَءَاهَا تَهۡتَزُّ كَأَنَّهَا جَآنّٞ وَلَّىٰ مُدۡبِرٗا وَلَمۡ يُعَقِّبۡۚ يَٰمُوسَىٰ لَا تَخَفۡ إِنِّي لَا يَخَافُ لَدَيَّ ٱلۡمُرۡسَلُونَ
Na itupe fimbo yako!» Akaitupa ikawa nyoka. Alipoiona inatikisika kwa ulaini kama vile nyoka mwepesi anavyojitikisa, alizunguka kukimbia na asiirudie. Hapo Mwenyezi Mungu Akamtuliza kwa neno Lake, «Ewe Mūsā! Usiogope. Hakika mimi hawaogopi mbele yangu wale niliowatuma na ujumbe wangu.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِلَّا مَن ظَلَمَ ثُمَّ بَدَّلَ حُسۡنَۢا بَعۡدَ سُوٓءٖ فَإِنِّي غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Isipokuwa yule aliyepitisha mpaka kwa kufanya dhambi kisha akatubia, akabadilisha toba njema baada ya dhambi baya, kwani mimi ni mwenye kumsamehe ni mwenye kumrehemu.» Basi asikate tamaa mtu yoyote na rehema ya Mwenyezi Mungu na msamaha Wake.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَأَدۡخِلۡ يَدَكَ فِي جَيۡبِكَ تَخۡرُجۡ بَيۡضَآءَ مِنۡ غَيۡرِ سُوٓءٖۖ فِي تِسۡعِ ءَايَٰتٍ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَقَوۡمِهِۦٓۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَوۡمٗا فَٰسِقِينَ
«Na utie mkono wako kwenye uwazi wa kanzu yako uliofunuliwa kifuani, utatoka ukiwa mweupe kama barafu, bila ya kuwa na mbalanga, ikiwa ni moja ya miujiza tisa, nayo, pamoja na huo mkono, ni fimbo, miaka ya ukame, upungufu wa matunda, mafuriko, nzige, chawa, vyura na damu, ili kukupa nguvu wewe katika ujumbe wako utakaoupeleka kwa Fir’awn na watu wake. Hakika wao walikuwa ni watu waliotoka nje ya amri ya Mwenyezi Mungu na kumkanusha.»
Arabic explanations of the Qur’an:
فَلَمَّا جَآءَتۡهُمۡ ءَايَٰتُنَا مُبۡصِرَةٗ قَالُواْ هَٰذَا سِحۡرٞ مُّبِينٞ
Miujiza hii ilipowajia, hali ya kuwa imefunuka wazi, inamfanya mwenye kuitazama auone uhakika wa yale inayoyatolea ushahidi, walisema, «Huu ni uchawi uliofunuka waziwazi.»
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: An-Naml
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis - Translations’ Index

Translated by Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr & Sh. Naser Khamis

close