Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis * - Translations’ Index


Translation of the meanings Surah: Al-Isrā’   Ayah:
إِلَّا رَحۡمَةٗ مِّن رَّبِّكَۚ إِنَّ فَضۡلَهُۥ كَانَ عَلَيۡكَ كَبِيرٗا
Lakini Mwenyezi Mungu Alikurehemu, Akaithibitisha moyoni mwako, hakika wema Wake juu yako ni mkubwa. Yeye Amekupa hii Qur’ani tukufu, Al-Maqām al-Maḥmūd (Kisimamo Kishukuriwacho) na mengineyo miongoni mwa yale ambayo Hakumpa yoyote katika viumbe.
Arabic explanations of the Qur’an:
قُل لَّئِنِ ٱجۡتَمَعَتِ ٱلۡإِنسُ وَٱلۡجِنُّ عَلَىٰٓ أَن يَأۡتُواْ بِمِثۡلِ هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ لَا يَأۡتُونَ بِمِثۡلِهِۦ وَلَوۡ كَانَ بَعۡضُهُمۡ لِبَعۡضٖ ظَهِيرٗا
Sema, «Lau wataafikiana majini na binadamu kujaribu kuleta mfano wa hii Qur’ani yenye kuelemea, hawataweza kuileta, hata kama watashirikiana na kusaidiana kufanya hivyo.»
Arabic explanations of the Qur’an:
وَلَقَدۡ صَرَّفۡنَا لِلنَّاسِ فِي هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ مِن كُلِّ مَثَلٖ فَأَبَىٰٓ أَكۡثَرُ ٱلنَّاسِ إِلَّا كُفُورٗا
Na tumewafafanulia watu katika hii Qur’ani kila aina ya mfano unaopasa kuzingatiwa, kwa njia ya kuwasimamishia hoja, ili waifuate na waitumie, lakini wengi wa watu walikataa isipokuwa ni kuipinga haki na kuzikanusha hoja za Mwenyezi Mungu na dalili Zake.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَقَالُواْ لَن نُّؤۡمِنَ لَكَ حَتَّىٰ تَفۡجُرَ لَنَا مِنَ ٱلۡأَرۡضِ يَنۢبُوعًا
Na Qur’ani ilipowaelemea washirikina na ikawashinda, waliingia kutaka miujiza kulingana na mapendeleo yao wakasema, «Hatutakuamini, ewe Muhammad, na hatutafanya vile unavyosema mpaka utupasulie kwenye ardhi ya Makkah chemchemu ya maji yenye kupita.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَوۡ تَكُونَ لَكَ جَنَّةٞ مِّن نَّخِيلٖ وَعِنَبٖ فَتُفَجِّرَ ٱلۡأَنۡهَٰرَ خِلَٰلَهَا تَفۡجِيرًا
«Au uwe na shamba lenye aina za mitende na mizabibu, na uifanye mito ni yenye kupita kati yake kwa wingi.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَوۡ تُسۡقِطَ ٱلسَّمَآءَ كَمَا زَعَمۡتَ عَلَيۡنَا كِسَفًا أَوۡ تَأۡتِيَ بِٱللَّهِ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ قَبِيلًا
«Au uiangushe mbingu juu yetu iwe vipande-vipande kama ulivyodai, au utuletee Mwenyezi Mungu na Malaika Wake tuwaone wametukabili waziwazi.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَوۡ يَكُونَ لَكَ بَيۡتٞ مِّن زُخۡرُفٍ أَوۡ تَرۡقَىٰ فِي ٱلسَّمَآءِ وَلَن نُّؤۡمِنَ لِرُقِيِّكَ حَتَّىٰ تُنَزِّلَ عَلَيۡنَا كِتَٰبٗا نَّقۡرَؤُهُۥۗ قُلۡ سُبۡحَانَ رَبِّي هَلۡ كُنتُ إِلَّا بَشَرٗا رَّسُولٗا
«Au uwe na nyumba ya dhahabu, au upande daraja za kukupaisha mbinguni, na hatutaamini kupaa kwako mpaka urudi ukiwa na kitabu kitokacho kwa Mwenyezi Mungu kilichofunguliwa tusome ndani yake kwamba wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kikweli.» Sema, ewe Mtume, kwa kushangaa juu ya ushindani wa makafiri hawa, «Kutakata na sifa za upungufu ni kwa Mola wangu! Kwani mimi ni nani, isipokuwa ni mja miongoni mwa waja Wake mwenye kufikisha ujumbe Wake? Basi vipi mimi nitaweza kuyafanya mnayoyataka?»
Arabic explanations of the Qur’an:
وَمَا مَنَعَ ٱلنَّاسَ أَن يُؤۡمِنُوٓاْ إِذۡ جَآءَهُمُ ٱلۡهُدَىٰٓ إِلَّآ أَن قَالُوٓاْ أَبَعَثَ ٱللَّهُ بَشَرٗا رَّسُولٗا
Na hakuna kilichowazuia makafiri kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na kuwatii, pindi ulipowajia wao ufafanuzi wa kutosha kutoka kwa Mwenyezi Mungu, isipokuwa ni kule kusema kwao kwa ujinga na kwa njia ya kukanusha, «Je, kwani Mwenyezi Mungu Ametumiliza Mtume miongoni mwa jinsi ya binadamu?»
Arabic explanations of the Qur’an:
قُل لَّوۡ كَانَ فِي ٱلۡأَرۡضِ مَلَٰٓئِكَةٞ يَمۡشُونَ مُطۡمَئِنِّينَ لَنَزَّلۡنَا عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ مَلَكٗا رَّسُولٗا
Waambie, ewe Muhammad, ukiwarudi washirikina kule kukanusha kwao kuwa Mtume ni miongoni mwa wanadamu, «Lau juu ya hii ardhi kulikuwa na Malaika wanatembea kwa kujituliza, tungaliwapelekea mtume miongoni mwa jinsi yao,» lakini watu wa ardhi ni wanadamu, basi mtume wa kupelekewa inatakiwa awe ni miongoni mwa jinsi yao, ili iwezekane kwao kuzungumza naye na kufahamu maneno yake.
Arabic explanations of the Qur’an:
قُلۡ كَفَىٰ بِٱللَّهِ شَهِيدَۢا بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۚ إِنَّهُۥ كَانَ بِعِبَادِهِۦ خَبِيرَۢا بَصِيرٗا
Waambie, «Inatosha kuwa Mwenyezi Mungu ni shahidi baina yangu mimi na nyinyi juu ya ukweli wangu na uhakika wa unabii wangu. Hakika Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, ni Mtambuzi wa hali za waja Wake ni Muoni wa matendo yao, na Atawalipa kwa hayo.»
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Al-Isrā’
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis - Translations’ Index

Translated by Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr & Sh. Naser Khamis

close