Check out the new design

ការបកប្រែអត្ថន័យនៃគម្ពីរគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស * - មាតិកានៃការបកប្រែ


ការបកប្រែអត្ថន័យ ជំពូក​: អាន់ណាហ្ពាក   វាក្យខណ្ឌ:

An-Naba

عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
Kuhusu kitu gani baadhi ya makafiri wa Kikureshi wanaulizana?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلۡعَظِيمِ
Wanaulizana kuhusu habari iliyo na uzito mkubwa kabisa,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ مُخۡتَلِفُونَ
nayo ni Qur’ani tukufu inayotoa habari za kufufuliwa ambako makafiri wa Kikureshi wana shaka nako na wanakukanusha.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Mambo sivyo kama wanavyodhania hawa washirikina. Hapo watajua hawa washirikina upeo wa kukanusha kwao na kitawadhihirikia waziwazi kile Atakachowatenda Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
ثُمَّ كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Kisha litahakikishika kwao jambo hilo na utahakikishika kwao ukweli wa yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kuhusu Qur’ani na kufufuliwa. Huu ni utisho na makemeo kwao.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَٰدٗا
Kwani hatukuwatandazia ardhi kama tandiko?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَٱلۡجِبَالَ أَوۡتَادٗا
Na Tukawafanyia majabali kuwa ni vigingi, ili isitisike nanyi?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَخَلَقۡنَٰكُمۡ أَزۡوَٰجٗا
Na Tukawaumba aina mbali-mbali, mume na mke.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتٗا
Na Tukafanya usingizi wenu ni mapumziko kwa viwiliwili vyenu: ndani yake mnatulia na kupumzika?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا
Na Tukaufanya usiku kuwa ni vazi, unawavisha giza lake na kuwafinika, kama nguo inavyomsitiri mwenye kuivaa.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَجَعَلۡنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشٗا
Na Tukaufanya mchana ni kipindi cha kutafuta maisha, mnaenea humo kwa ajili ya maisha yenu na mnatembea humo kwa ajili ya maslahi yenu?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَبَنَيۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعٗا شِدَادٗا
Na Tukajenga juu yenu mbingu saba, madhubuti jengo lake, lilioumbwa kwa uzuri, halina mapasuko wala nyufa?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَجَعَلۡنَا سِرَاجٗا وَهَّاجٗا
Na Tukalifanya jua kuwa ni taa iwakayo na kung’ara?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡمُعۡصِرَٰتِ مَآءٗ ثَجَّاجٗا
Na Tukateremsha kutoka kwenye mawingu yanyeshayo maji yamiminikayo kwa wingi,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
لِّنُخۡرِجَ بِهِۦ حَبّٗا وَنَبَاتٗا
ili Tutoe kwa maji hayo nafaka inayoliwa na watu,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَجَنَّٰتٍ أَلۡفَافًا
nyasi zinazoliwa na wanyama na miti iliyosongamana kwa kutawanyika tagaa zake?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ كَانَ مِيقَٰتٗا
Hakika Siku ya Uamuzi kati ya viumbe,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَتَأۡتُونَ أَفۡوَاجٗا
nayo ni Siku ya Kiyama, imekuwa ni wakati na ahadi iliyowekewa muda maalimu kwa watu wa mwanzo na wa mwisho.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٰبٗا
Na zikafunguliwa mbingu zikawa ni zenye milango mingi kwa ajili ya kuteremka Malaika.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا
Na yakalipuliwa majabali baada ya kuwa yamekita, yakawa ni kama mangati.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا
Hakika Jahanamu, Siku Hiyo, itawalindiza wenye ukafiri ambao Moto huo umeandaliwa wao.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابٗا
Kwa makafiri ndio marejeo.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحۡقَابٗا
Watabakia humo muda mrefu ufuatanao, usiokoma.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرۡدٗا وَلَا شَرَابًا
Hawatakula humo chochote kitakachozizimisha joto la moto kwao.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِلَّا حَمِيمٗا وَغَسَّاقٗا
Wala kinywaji kitakachowaondolea kiu yao. Isipokuwa maji moto na usaha wa watu wa motoni.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
جَزَآءٗ وِفَاقًا
Watakuwa wanalipwa kwa hilo malipo ya sawa yanayolingana na vitendo vyao walivyovitenda duniani
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِنَّهُمۡ كَانُواْ لَا يَرۡجُونَ حِسَابٗا
Hakika wao walikuwa hawaiyogopi Siku ya Hesabu, na kwa hivyo hawakujitayarisha nayo kwa kufanya matendo ya kuwafaa.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابٗا
Na waliyakanusha waziwazi yaliyoletwa na Mitume.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا
Na kila kitu Tulikijua na Tukakiandika katika Ubao uliohifadhiwa (Al-Lawḥ Al-Maḥfūd).
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَذُوقُواْ فَلَن نَّزِيدَكُمۡ إِلَّا عَذَابًا
Basi Onjeni, enyi makafiri, hayo yakiwa ni malipo ya vitendo vyenu, Hatutawazidishia isipokuwa adhabu juu ya adhabu yenu.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
 
ការបកប្រែអត្ថន័យ ជំពូក​: អាន់ណាហ្ពាក
មាតិកានៃជំពូក លេខ​ទំព័រ
 
ការបកប្រែអត្ថន័យនៃគម្ពីរគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស - មាតិកានៃការបកប្រែ

ការបកប្រែដោយលោកបណ្ឌិតអាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ អាពូហ្ពើកើរ និងលោកណាសៀរ ខមុីស

បិទ