Check out the new design

Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassarar Sawahil - Cibiyar fassara ta Ruwwad * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Fassarar Ma'anoni Sura: Al'ifidar   Aya:

Al-Infitar

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ
Mbingu itakapochanika.
Tafsiran larabci:
وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ
Na nyota zitakapotawanyika.
Tafsiran larabci:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ
Na bahari zitakapopasuliwa.
Tafsiran larabci:
وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ
Na makaburi yatakapofukuliwa.
Tafsiran larabci:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ
Hapo kila nafsi itajua ilichotanguliza, na ilichobakisha nyuma.
Tafsiran larabci:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ
Ewe mwanadamu! Nini kilichokudanganya ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
Tafsiran larabci:
ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Aliyekuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha.
Tafsiran larabci:
فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
Katika sura yoyote aliyoipenda akakujenga.
Tafsiran larabci:
كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
Tafsiran larabci:
وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu.
Tafsiran larabci:
كِرَامٗا كَٰتِبِينَ
Waandishi wenye heshima.
Tafsiran larabci:
يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ
Wanayajua mnayoyatenda.
Tafsiran larabci:
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
Tafsiran larabci:
وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni.
Tafsiran larabci:
يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Wataingia humo Siku ya Malipo.
Tafsiran larabci:
وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ
Na hawatoacha kuwamo humo.
Tafsiran larabci:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Na nini kitakachokujulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
Tafsiran larabci:
ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Tena nini kitakachokujulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
Tafsiran larabci:
يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ
Siku ambayo nafsi haitakuwa na mamalaka yoyote juu ya nafsi nyingine; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Sura: Al'ifidar
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassarar Sawahil - Cibiyar fassara ta Ruwwad - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

Wani gungu na cibiyar fassara ta Ruwad ne suka fassarasu tare da haɗin gwiwar Ƙungiyar Da'awa ta Rabwah da Kungiyar hidimtawa abinda Musulunci ya kunsa da yaruka

Rufewa