Check out the new design

Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da harshen Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Sura: Al'naml   Aya:
إِنِّي وَجَدتُّ ٱمۡرَأَةٗ تَمۡلِكُهُمۡ وَأُوتِيَتۡ مِن كُلِّ شَيۡءٖ وَلَهَا عَرۡشٌ عَظِيمٞ
«Mimi nimemkuta mwanamke anawatawala watu wa Saba ’, na amepatiwa kila kitu katika mahitaji ya utawala wa kidunia, na ana kitanda cha heshima kubwa anakalia juu yake kuendesha mambo ya ufalme wake.
Tafsiran larabci:
وَجَدتُّهَا وَقَوۡمَهَا يَسۡجُدُونَ لِلشَّمۡسِ مِن دُونِ ٱللَّهِ وَزَيَّنَ لَهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَعۡمَٰلَهُمۡ فَصَدَّهُمۡ عَنِ ٱلسَّبِيلِ فَهُمۡ لَا يَهۡتَدُونَ
«Nimemkuta Yeye na watu wake wanaabudu jua, wakiacha kumuabudu Mwenyezi Mungu. Na Shetani Amewapambia matendo yao mabaya waliokuwa wakiyafanya, akawaepusha na kumuamini Mwenyezi Mungu na kumpwekesha, hivyo basi wao hawaongoki kuelekea kwa Mwenyezi Mungu, kumpwekesha na kumuabudu Peke Yake.»
Tafsiran larabci:
أَلَّاۤ يَسۡجُدُواْۤ لِلَّهِ ٱلَّذِي يُخۡرِجُ ٱلۡخَبۡءَ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَيَعۡلَمُ مَا تُخۡفُونَ وَمَا تُعۡلِنُونَ
Shetani amewapambia hilo, ili wasimsujudie Mwenyezi Mungu Ambaye Anakitoa kilichofichwa na kufinikwa mbinguni na ardhini miongoni mwa mvua, mimea na visivyokuwa hivyo, na Anayajua mnayoyafanya kwa siri na mnayoyafanya kwa dhahiri.
Tafsiran larabci:
ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ رَبُّ ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡعَظِيمِ۩
Mwenyezi Mungu, Ambaye hakuna muabudiwa anayestahiki ibada isipokuwa Yeye, ni Mola wa ‘Arsh iliyo kubwa ambayo ni kubwa kuliko viumbe vyote.
Tafsiran larabci:
۞ قَالَ سَنَنظُرُ أَصَدَقۡتَ أَمۡ كُنتَ مِنَ ٱلۡكَٰذِبِينَ
Sulaymān alisema kumwambia hud-hud, «Tutaichunguza habari uliyotuletea tujue: unasema kweli katika hiyo au umekuwa ni katika warongo ndani yake?
Tafsiran larabci:
ٱذۡهَب بِّكِتَٰبِي هَٰذَا فَأَلۡقِهۡ إِلَيۡهِمۡ ثُمَّ تَوَلَّ عَنۡهُمۡ فَٱنظُرۡ مَاذَا يَرۡجِعُونَ
Enda na barua yangu hii kwa watu wa Saba’ uwapatie, kisha jiepushe kando na wao ukiwa karibu nao mahali unapoweza kusikia maneno yao na uyatie akilini maneno yatakayopitika baina yao.»
Tafsiran larabci:
قَالَتۡ يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡمَلَؤُاْ إِنِّيٓ أُلۡقِيَ إِلَيَّ كِتَٰبٞ كَرِيمٌ
Hud-hud alienda akamrushia malkia ile barua. Papo hapo akaisoma na akawakasunya watukufu wa watu wake, na akamsikia akisema, «Mimi nimefikiwa na barua tukufu yenye cheo kutoka kwa mtu mkubwa wa cheo.»
Tafsiran larabci:
إِنَّهُۥ مِن سُلَيۡمَٰنَ وَإِنَّهُۥ بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
Kisha akayaeleza yaliyomo ndani akasema, «Hiyo inatoka kwa Sulaymān, nayo imeanza na ‘Bi ism Allāh al-Rahmān al-Rahīm» (Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwenye kuwarehemu wema na waovu ulimwenguni, Mwenye kuwarehemu wema watupu kesho Akhera)
Tafsiran larabci:
أَلَّا تَعۡلُواْ عَلَيَّ وَأۡتُونِي مُسۡلِمِينَ
Msifanye kiburi wala msijifanye wakubwa mkakataa kuyakubali haya ninayowalingania. Na njooni kwangu mkiwa ni wenye kukubali upweke wa Mwenyezi Mungu na kujisalimisha Kwake kwa utiifu.»
Tafsiran larabci:
قَالَتۡ يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡمَلَؤُاْ أَفۡتُونِي فِيٓ أَمۡرِي مَا كُنتُ قَاطِعَةً أَمۡرًا حَتَّىٰ تَشۡهَدُونِ
Akasema, «Enyi watukufu! Nipeni shauri kuhusu jambo hili. Sikuwa mimi ni mwenye kuamua jambo isipokuwa mbele yenu na kwa ushauri wenu.»
Tafsiran larabci:
قَالُواْ نَحۡنُ أُوْلُواْ قُوَّةٖ وَأُوْلُواْ بَأۡسٖ شَدِيدٖ وَٱلۡأَمۡرُ إِلَيۡكِ فَٱنظُرِي مَاذَا تَأۡمُرِينَ
Wakasema kumjibu ,»Sisi ni wenye nguvu wa idadi na silaha, na ni watu wa utetezi na ushujaa katika vita vikali, na uamuzi ni wako, na wewe ndiye mwenye maoni, basi fikiria unatuamrisha nini. Sisi ni wenye kusikiliza maneno yako na ni watiifu kwako.»
Tafsiran larabci:
قَالَتۡ إِنَّ ٱلۡمُلُوكَ إِذَا دَخَلُواْ قَرۡيَةً أَفۡسَدُوهَا وَجَعَلُوٓاْ أَعِزَّةَ أَهۡلِهَآ أَذِلَّةٗۚ وَكَذَٰلِكَ يَفۡعَلُونَ
Akasema akiwatahadharisha kukabiliana na Sulaymān kwa uadui na akiwaelezea mwisho mbaya wa kupigana, «Kwa hakika, wafalme wakiingia na majeshi yao kwenye mji kwa nguvu na ushindi, wanauharibu, wanawafanya watukufu wake kuwa wanyonge, wanauwa na wanachukua mateka. Na hii ndiyo desturi yao inayoendelea na inayojikita ili kuwafanya watu wawaogope.
Tafsiran larabci:
وَإِنِّي مُرۡسِلَةٌ إِلَيۡهِم بِهَدِيَّةٖ فَنَاظِرَةُۢ بِمَ يَرۡجِعُ ٱلۡمُرۡسَلُونَ
Na mimi nitamtumia Sulaymān tunu iliyokusanya mali ya thamani ili kufanya urafiki naye kwayo, na nitangojea watarudi na nini hao wajumbe.»
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Sura: Al'naml
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da harshen Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

Dr. Abdullahi Muhammad Abubakar da Sheikh Nasir Khamis suka fassarata.

Rufewa