Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Rowad Translation Center * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Surah: An-Nisā’   Ayah:
مَّن يُطِعِ ٱلرَّسُولَ فَقَدۡ أَطَاعَ ٱللَّهَۖ وَمَن تَوَلَّىٰ فَمَآ أَرۡسَلۡنَٰكَ عَلَيۡهِمۡ حَفِيظٗا
Mwenye kumtii Mtume, basi hakika amemtii Mwenyezi Mungu. Na mwenye kugeuka, basi Sisi hatukukutuma uwe mlinzi juu yao.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَيَقُولُونَ طَاعَةٞ فَإِذَا بَرَزُواْ مِنۡ عِندِكَ بَيَّتَ طَآئِفَةٞ مِّنۡهُمۡ غَيۡرَ ٱلَّذِي تَقُولُۖ وَٱللَّهُ يَكۡتُبُ مَا يُبَيِّتُونَۖ فَأَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِۚ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ وَكِيلًا
Na wanasema: 'Tunatii.' Lakini wanapotoka kule uliko, kundi moja miongoni mwao hupanga njama usiku kinyume na unayoyasema. Na Mwenyezi Mungu anayaandika yote hayo wanayoyapangia njama za usiku. Basi wape mgongo, na umtegemee Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa Mtegemewa.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَفَلَا يَتَدَبَّرُونَ ٱلۡقُرۡءَانَۚ وَلَوۡ كَانَ مِنۡ عِندِ غَيۡرِ ٱللَّهِ لَوَجَدُواْ فِيهِ ٱخۡتِلَٰفٗا كَثِيرٗا
Kwani hawaizingatii hii Qur-ani? Na lau kuwa ingetoka kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, bila ya shaka wangelikuta ndani yake hitilafu nyingi.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِذَا جَآءَهُمۡ أَمۡرٞ مِّنَ ٱلۡأَمۡنِ أَوِ ٱلۡخَوۡفِ أَذَاعُواْ بِهِۦۖ وَلَوۡ رَدُّوهُ إِلَى ٱلرَّسُولِ وَإِلَىٰٓ أُوْلِي ٱلۡأَمۡرِ مِنۡهُمۡ لَعَلِمَهُ ٱلَّذِينَ يَسۡتَنۢبِطُونَهُۥ مِنۡهُمۡۗ وَلَوۡلَا فَضۡلُ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ وَرَحۡمَتُهُۥ لَٱتَّبَعۡتُمُ ٱلشَّيۡطَٰنَ إِلَّا قَلِيلٗا
Na linapowajia jambo lolote linalohusiana na amani au hofu, wao wanalitangaza. Na lau kuwa wangelipeleka kwa Mtume na kwa wenye mamlaka kati yao, wale wanaochunguza miongoni mwao wangelijua. Na lau kuwa si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yenu na rehema yake, mngelimfuata Shetani isipokuwa wachache tu.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ لَا تُكَلَّفُ إِلَّا نَفۡسَكَۚ وَحَرِّضِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ عَسَى ٱللَّهُ أَن يَكُفَّ بَأۡسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ وَٱللَّهُ أَشَدُّ بَأۡسٗا وَأَشَدُّ تَنكِيلٗا
Basi pigana vita katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Hutwikwi isipokuwa nafsi yako tu. Na wahimize Waumini. Huenda Mwenyezi Mungu akayazuia mashambulizi ya wale waliokufuru. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mkali zaidi wa kushambulia, na Mkali zaidi wa kutesa.
Arabic explanations of the Qur’an:
مَّن يَشۡفَعۡ شَفَٰعَةً حَسَنَةٗ يَكُن لَّهُۥ نَصِيبٞ مِّنۡهَاۖ وَمَن يَشۡفَعۡ شَفَٰعَةٗ سَيِّئَةٗ يَكُن لَّهُۥ كِفۡلٞ مِّنۡهَاۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ مُّقِيتٗا
Mwenye kufanya uombezi mzuri, ana fungu lake katika hayo. Na mwenye kufanya uombezi mbaya, naye ana sehemu yake katika hayo. Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye uwezo na ujuzi juu ya kila kitu.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٖ فَحَيُّواْ بِأَحۡسَنَ مِنۡهَآ أَوۡ رُدُّوهَآۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٍ حَسِيبًا
Na mnapoamkiwa kwa maamkizi yoyote, basi itikieni kwa yaliyo mazuri zaidi kuliko hayo, au yarejesheni hayo hayo. Hakika, Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuhesabu kila kitu.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: An-Nisā’
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Rowad Translation Center - Translations’ Index

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

close