Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Rowad Translation Center * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Surah: Sād   Ayah:
وَقَالُواْ مَا لَنَا لَا نَرَىٰ رِجَالٗا كُنَّا نَعُدُّهُم مِّنَ ٱلۡأَشۡرَارِ
Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao tukiwahisabu ndio katika waovu?
Arabic explanations of the Qur’an:
أَتَّخَذۡنَٰهُمۡ سِخۡرِيًّا أَمۡ زَاغَتۡ عَنۡهُمُ ٱلۡأَبۡصَٰرُ
Tulikosea tulipowafanyia masihara, au macho yetu tu hayawaoni?
Arabic explanations of the Qur’an:
إِنَّ ذَٰلِكَ لَحَقّٞ تَخَاصُمُ أَهۡلِ ٱلنَّارِ
Hakika hayo bila ya shaka ndiyo mahasimiano ya watu wa Motoni.
Arabic explanations of the Qur’an:
قُلۡ إِنَّمَآ أَنَا۠ مُنذِرٞۖ وَمَا مِنۡ إِلَٰهٍ إِلَّا ٱللَّهُ ٱلۡوَٰحِدُ ٱلۡقَهَّارُ
Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana mungu ila Mwenyezi Mungu Mmoja, Mtenda nguvu.
Arabic explanations of the Qur’an:
رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡغَفَّٰرُ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake, Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe.
Arabic explanations of the Qur’an:
قُلۡ هُوَ نَبَؤٌاْ عَظِيمٌ
Sema: Hii ni habari kubwa kabisa.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَنتُمۡ عَنۡهُ مُعۡرِضُونَ
Ambayo nyinyi mnaipuuza.
Arabic explanations of the Qur’an:
مَا كَانَ لِيَ مِنۡ عِلۡمِۭ بِٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰٓ إِذۡ يَخۡتَصِمُونَ
Sikuwa na elimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipokuwa wakishindana.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِن يُوحَىٰٓ إِلَيَّ إِلَّآ أَنَّمَآ أَنَا۠ نَذِيرٞ مُّبِينٌ
Haikufunuliwa kwangu isipokuwa ya kwamba hakika mimi ni mwonyaji dhahiri.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَٰٓئِكَةِ إِنِّي خَٰلِقُۢ بَشَرٗا مِّن طِينٖ
Mola wako Mlezi alipowaambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَإِذَا سَوَّيۡتُهُۥ وَنَفَخۡتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُواْ لَهُۥ سَٰجِدِينَ
Na nitakapomkamilisha na kumpulizia roho inayotokana nami, basi muangukieni kwa kumtii.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَسَجَدَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ كُلُّهُمۡ أَجۡمَعُونَ
Basi wakasujudu Malaika wote pamoja.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِلَّآ إِبۡلِيسَ ٱسۡتَكۡبَرَ وَكَانَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Isipokuwa Iblisi; alijivuna na akawa katika makafiri.
Arabic explanations of the Qur’an:
قَالَ يَٰٓإِبۡلِيسُ مَا مَنَعَكَ أَن تَسۡجُدَ لِمَا خَلَقۡتُ بِيَدَيَّۖ أَسۡتَكۡبَرۡتَ أَمۡ كُنتَ مِنَ ٱلۡعَالِينَ
Mwenyezi Mungu akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilichokuzuia kumtii yule niliyemuumba kwa mikono yangu? Je, umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?
Arabic explanations of the Qur’an:
قَالَ أَنَا۠ خَيۡرٞ مِّنۡهُ خَلَقۡتَنِي مِن نَّارٖ وَخَلَقۡتَهُۥ مِن طِينٖ
Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo.
Arabic explanations of the Qur’an:
قَالَ فَٱخۡرُجۡ مِنۡهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٞ
Akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umelaanika.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِنَّ عَلَيۡكَ لَعۡنَتِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلدِّينِ
Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo.
Arabic explanations of the Qur’an:
قَالَ رَبِّ فَأَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watakayofufuliwa viumbe.
Arabic explanations of the Qur’an:
قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ
Mwenyezi Mungu akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa waliopewa muhula.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ
Mpaka siku ya wakati maalumu.
Arabic explanations of the Qur’an:
قَالَ فَبِعِزَّتِكَ لَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ
Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa wale waja wako miongoni mwao waliohitariwa.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Sād
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Rowad Translation Center - Translations’ Index

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

close