Check out the new design

Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Rowad Translation Center * - Translations’ Index

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Translation of the meanings Surah: Ash-Shu‘arā’   Ayah:

Ash-Shu'ara

طسٓمٓ
Tw'a Siin Miim.[1]
[1] Herufi hizi "Tw'aa, Sin, Miim" na herufi nyinginezo za mkato zilizo mwanzoni mwa sura mbalimbali zinaonyesha hali ya ushindi wa Qur-ani. Kwani, washirikina walipewa changamoto kwayo, lakini wakashindwa na hawakuweza kuipinga, ilhali inajumuisha herufi hizi zinazounda lugha ya Kiarabu. Kwa hivyo, kutoweza kwa Waarabu kuleta kitu kama hicho - ingawa walikuwa ndio watu wenye ufasaha zaidi - kunaonyesha kwamba Qur-ani ni ufunuo (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Arabic explanations of the Qur’an:
تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ
Hizi ni Aya za Kitabu kinachobainisha.
Arabic explanations of the Qur’an:
لَعَلَّكَ بَٰخِعٞ نَّفۡسَكَ أَلَّا يَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ
Huenda ukaihiliki nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِن نَّشَأۡ نُنَزِّلۡ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةٗ فَظَلَّتۡ أَعۡنَٰقُهُمۡ لَهَا خَٰضِعِينَ
Tungependa, tungeliwateremshia kutoka mbinguni Ishara zikashinda zimezinyenyekea shingo zao.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن ذِكۡرٖ مِّنَ ٱلرَّحۡمَٰنِ مُحۡدَثٍ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهُ مُعۡرِضِينَ
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman (Mwingi wa rehema), isipokuwa wao huupa mgongo.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَقَدۡ كَذَّبُواْ فَسَيَأۡتِيهِمۡ أَنۢبَٰٓؤُاْ مَا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Kwa yakini wamekwishakanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia habari za yale waliyokuwa wakiyafanyia stihizai.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَمۡ أَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجٖ كَرِيمٍ
Je, hawakuiona ardhi, ni mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
Arabic explanations of the Qur’an:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِذۡ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئۡتِ ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na Mola wako Mlezi, alipomwita Musa, akamwambia: Nenda kwa kaumu madhalimu.
Arabic explanations of the Qur’an:
قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَۚ أَلَا يَتَّقُونَ
Kaumu wa Firauni. Kwani hawamchi Mwenyezi Mungu?
Arabic explanations of the Qur’an:
قَالَ رَبِّ إِنِّيٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi, hakika mimi ninachelea kwamba watanikadhibisha.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَيَضِيقُ صَدۡرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرۡسِلۡ إِلَىٰ هَٰرُونَ
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَلَهُمۡ عَلَيَّ ذَنۢبٞ فَأَخَافُ أَن يَقۡتُلُونِ
Na wao wana dhambi niliyowafanyia, kwa hivyo ninahofu wanaweza kuniua.
Arabic explanations of the Qur’an:
قَالَ كَلَّاۖ فَٱذۡهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسۡتَمِعُونَ
Akasema: Sivyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَأۡتِيَا فِرۡعَوۡنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Basi nendeni kwa Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Arabic explanations of the Qur’an:
أَنۡ أَرۡسِلۡ مَعَنَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Kwamba: Waachilie Wana wa Israili waende pamoja nasi.
Arabic explanations of the Qur’an:
قَالَ أَلَمۡ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدٗا وَلَبِثۡتَ فِينَا مِنۡ عُمُرِكَ سِنِينَ
(Firauni) akasema: Je, sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa miongoni mwetu katika umri wako miaka mingi?
Arabic explanations of the Qur’an:
وَفَعَلۡتَ فَعۡلَتَكَ ٱلَّتِي فَعَلۡتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na ukatenda kitendo chako ulichotenda, nawe ukawa miongoni mwa wenye kukufuru?
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Ash-Shu‘arā’
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Rowad Translation Center - Translations’ Index

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

close