Check out the new design

আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - শ্বাহিলি অনুবাদ- ৰুওৱাদ অনুবাদ চেণ্টাৰ * - অনুবাদসমূহৰ সূচীপত্ৰ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

অৰ্থানুবাদ ছুৰা: আত-তুৰ   আয়াত:

At-Tur

وَٱلطُّورِ
Ninaapa kwa mlima wa T'ur.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ
Na Kitabu kilichoandikwa.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ
Katika ngozi iliyokunjuliwa.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ
Na kwa Nyumba iliyojengwa.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ
Na kwa dari iliyonyanyuliwa.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ
Na kwa bahari iliyojazwa.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ
Hapana wa kuizuia.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا
Siku zitakapotikisika mbingu kwa mtikiso.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Basi ole wao siku hiyo hao wanaokadhibisha.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا
Siku watakaposukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mliokuwa mkiukadhibisha!
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَفَسِحۡرٌ هَٰذَآ أَمۡ أَنتُمۡ لَا تُبۡصِرُونَ
Je, huu ni uchawi, au hamwoni tu?
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
ٱصۡلَوۡهَا فَٱصۡبِرُوٓاْ أَوۡ لَا تَصۡبِرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡكُمۡۖ إِنَّمَا تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyokuwa mkiyatenda.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَنَعِيمٖ
Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na neema.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ وَوَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ
Wakifurahi kwa yale aliyowapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyokuwa mkiyatenda.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٖ مَّصۡفُوفَةٖۖ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyopangwa kwa safu. Na tutawaoza mahurulaini.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱتَّبَعَتۡهُمۡ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلۡحَقۡنَا بِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَمَآ أَلَتۡنَٰهُم مِّنۡ عَمَلِهِم مِّن شَيۡءٖۚ كُلُّ ٱمۡرِيِٕۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٞ
Na wale walioamini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani, tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alichokichuma.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَأَمۡدَدۡنَٰهُم بِفَٰكِهَةٖ وَلَحۡمٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ
Na tutawapa matunda, na nyama kama watakavyopenda.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأۡسٗا لَّا لَغۡوٞ فِيهَا وَلَا تَأۡثِيمٞ
Watapeana humo bilauri zisizo na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
۞ وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ غِلۡمَانٞ لَّهُمۡ كَأَنَّهُمۡ لُؤۡلُؤٞ مَّكۡنُونٞ
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ
Wataelekeana wakiulizana.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
قَالُوٓاْ إِنَّا كُنَّا قَبۡلُ فِيٓ أَهۡلِنَا مُشۡفِقِينَ
Waseme: Hakika tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa mno.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda mbali adhabu ya upepo wa Moto.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلُ نَدۡعُوهُۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡبَرُّ ٱلرَّحِيمُ
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwingi wa kurehemu.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَذَكِّرۡ فَمَآ أَنتَ بِنِعۡمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٖ وَلَا مَجۡنُونٍ
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ يَقُولُونَ شَاعِرٞ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيۡبَ ٱلۡمَنُونِ
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
قُلۡ تَرَبَّصُواْ فَإِنِّي مَعَكُم مِّنَ ٱلۡمُتَرَبِّصِينَ
Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ تَأۡمُرُهُمۡ أَحۡلَٰمُهُم بِهَٰذَآۚ أَمۡ هُمۡ قَوۡمٞ طَاغُونَ
Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُۥۚ بَل لَّا يُؤۡمِنُونَ
Au ndiyo wanasema: 'Ameitunga hii!' Bali basi tu hawaamini!
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَلۡيَأۡتُواْ بِحَدِيثٖ مِّثۡلِهِۦٓ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ
Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ خُلِقُواْ مِنۡ غَيۡرِ شَيۡءٍ أَمۡ هُمُ ٱلۡخَٰلِقُونَ
Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ خَلَقُواْ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ
Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana yakini.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ عِندَهُمۡ خَزَآئِنُ رَبِّكَ أَمۡ هُمُ ٱلۡمُصَۜيۡطِرُونَ
Au wanazo hazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ لَهُمۡ سُلَّمٞ يَسۡتَمِعُونَ فِيهِۖ فَلۡيَأۡتِ مُسۡتَمِعُهُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ
Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja iliyo wazi!
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ لَهُ ٱلۡبَنَٰتُ وَلَكُمُ ٱلۡبَنُونَ
Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ
Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ
Au wanayo elimu ya ghaibu, nao wameandika?
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ يُرِيدُونَ كَيۡدٗاۖ فَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ هُمُ ٱلۡمَكِيدُونَ
Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao waliokufuru ndio watakaotegeka.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
أَمۡ لَهُمۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِۚ سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشۡرِكُونَ
Au wanaye mungu asiyekuwa Mwenyezi Mungu? Ametakasika Mwenyezi Mungu mbali na hao wanaowashirikisha naye.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَإِن يَرَوۡاْ كِسۡفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ سَاقِطٗا يَقُولُواْ سَحَابٞ مَّرۡكُومٞ
Na hata wangeona pande linatoka mbinguni linaanguka wangesema: Ni mawingu yaliyobebana.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
فَذَرۡهُمۡ حَتَّىٰ يُلَٰقُواْ يَوۡمَهُمُ ٱلَّذِي فِيهِ يُصۡعَقُونَ
Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapohilikishwa.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
يَوۡمَ لَا يُغۡنِي عَنۡهُمۡ كَيۡدُهُمۡ شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ
Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ عَذَابٗا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Na hakika wale waliodhulumu watapata adhabu nyingine isiyokuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعۡيُنِنَاۖ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ
Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu,
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَإِدۡبَٰرَ ٱلنُّجُومِ
Na usiku pia mtakase, na zinapokuchwa nyota.
আৰবী তাফছীৰসমূহ:
 
অৰ্থানুবাদ ছুৰা: আত-তুৰ
ছুৰাৰ তালিকা পৃষ্ঠা নং
 
আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - শ্বাহিলি অনুবাদ- ৰুওৱাদ অনুবাদ চেণ্টাৰ - অনুবাদসমূহৰ সূচীপত্ৰ

অনুবাদ কৰিছে جمعية الدعوة بالربوة আৰু جمعية خدمة المحتوى الإسلامي باللغاتৰ সহযোগত মৰ্কজ ৰুৱাদুত তাৰ্জামাৰ অনুবাদক গোষ্ঠীয়ে।

বন্ধ