Check out the new design

የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የስዋሂሊ ትርጉም - በዐብደላህ ሙሐመድ እና በናስር ኸሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሷድ   አንቀጽ:
وَوَهَبۡنَا لَهُۥٓ أَهۡلَهُۥ وَمِثۡلَهُم مَّعَهُمۡ رَحۡمَةٗ مِّنَّا وَذِكۡرَىٰ لِأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ
Tukamuondolea shida yake na tukamtukuza, na tukamtunukia watu wake : mke na watoto, na tukamuongezea wana na wajukuu mfano wao. Yote hayo yalikuwa ni huruma kutoka kwetu na takrima kwake kwa uvumilivu wake, na pia ni mazingatio kwa wenye akili timamu, wapate kujua kwamba mwisho wa subira ni faraja na kuondokewa na shida.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَخُذۡ بِيَدِكَ ضِغۡثٗا فَٱضۡرِب بِّهِۦ وَلَا تَحۡنَثۡۗ إِنَّا وَجَدۡنَٰهُ صَابِرٗاۚ نِّعۡمَ ٱلۡعَبۡدُ إِنَّهُۥٓ أَوَّابٞ
Na tukamwambia yeye, «chukua kwa mkono wako mrundiko wa nyasi au mfano wake umpige nao mke wako, ili utekeleze yamini lako na usilivunje. Kwani yeye alikuwa ameapa kuwa atampiga mbati mia moja Mwenyezi Mungu Akimponyesha, alipomkasirikia mkewe kwa jambo dogo alipokuwa mgonjwa. Na alikuwa ni mwanamke mwema na Mwenyezi Mungu Akamhurumia yeye na Akamhurumia mumewe kwa uamuzi huu. Hakika sisi tumemkuta Ayyūb ni mvumilivu katika mitihani. Mja bora ni yeye, kwani yeye ni mwingi wa kurudi kwenye utiifu wa Mola wake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱذۡكُرۡ عِبَٰدَنَآ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ أُوْلِي ٱلۡأَيۡدِي وَٱلۡأَبۡصَٰرِ
Wakumbuke, ewe Mtume, waja wetu na Manabii wetu: Ibrāhīm, Is’ḥāq na Ya’qūb. Hakika wao ni watu wenye nguvu katika kumtii Mwenyezi Mungu na ujuzi katika Dini Yake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّآ أَخۡلَصۡنَٰهُم بِخَالِصَةٖ ذِكۡرَى ٱلدَّارِ
Sisi tumewahusisha wao kwa jambo kubwa ambalo ni mahsusi kwao, kwa kuwa tumejaalia ukumbusho wa Nyumba ya Akhera uko ndani ya nyoyo zao, na kwa hivyo wakaifanyia kazi kwa kututii sisi na wakawalingania watu kwenye jambo hilo na kuwakumbusha.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَإِنَّهُمۡ عِندَنَا لَمِنَ ٱلۡمُصۡطَفَيۡنَ ٱلۡأَخۡيَارِ
Na kwa hakika, wao kwetu sisi ni miongoni mwa wale tuliowachagua ili watutii na tuliowateua kubeba ujumbe wetu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱذۡكُرۡ إِسۡمَٰعِيلَ وَٱلۡيَسَعَ وَذَا ٱلۡكِفۡلِۖ وَكُلّٞ مِّنَ ٱلۡأَخۡيَارِ
Wakumbuke, ewe Mtume, waja wetu: Ismā'īl, Ilyasa' na Dhulkifl kwa utajo mzuri sana. Na kila mmoja miongoni mwao ni katika watu wema ambao Mwenyezi Mungu Aliwachagua miongoni mwa viumbe na Akawachagulia hali na sifa kamilifu kabisa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
هَٰذَا ذِكۡرٞۚ وَإِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ لَحُسۡنَ مَـَٔابٖ
Hii Qur’ani ni utajo na utukufu kwako, ewe Mtume, na kwa watu wako. Na wale watu wa uchaji Mwenyezi Mungu na utiifu Kwake watakuwa na mwisho mwema kwetu sisi
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
جَنَّٰتِ عَدۡنٖ مُّفَتَّحَةٗ لَّهُمُ ٱلۡأَبۡوَٰبُ
kwenye Pepo za kukaa daima, milango yake ikiwa tayari imefunguliwa kwa ajili yao,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
مُتَّكِـِٔينَ فِيهَا يَدۡعُونَ فِيهَا بِفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ وَشَرَابٖ
watakuwa ni wenye kutegemea kwenye Pepo hizo juu ya viti vya fahari vilivyopambwa, watataka na kupatiwa kila wanachokitamani miongoni mwa aina nyingi za matunda na vinywaji, kutokana na kila ambacho nafsi zao zitakitamani na macho yao yatapendezwa nacho.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
۞ وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ أَتۡرَابٌ
Na huko watakuwa nao wanawake ambao macho yao yanawatazama waume zao tu hali wakiwa marika na wao kimiaka.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
هَٰذَا مَا تُوعَدُونَ لِيَوۡمِ ٱلۡحِسَابِ
Starehe hii ndiyo ile mliokuwa mkiahidiwa, enyi wachamungu, Siku ya Kiyama.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّ هَٰذَا لَرِزۡقُنَا مَا لَهُۥ مِن نَّفَادٍ
Hiyo ndiyo riziki yetu tuliyowaandalia nyinyi, haina kumalizika wala kukatika.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
هَٰذَاۚ وَإِنَّ لِلطَّٰغِينَ لَشَرَّ مَـَٔابٖ
Hayo, yaliyotangulia kutajwa sifa zake, ni ya wachamungu. Ama wale wenye kuruka mpaka na kuingia ukafirini na maasi, wao watakuwa na marejeo maovu kabisa na mwisho mbaya sana,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
جَهَنَّمَ يَصۡلَوۡنَهَا فَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ
nao ni Moto ambao ndani yake wataadhibiwa, utawafinika pande zao zote, basi tandiko baya mno ni tandiko lao.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
هَٰذَا فَلۡيَذُوقُوهُ حَمِيمٞ وَغَسَّاقٞ
Adhabu hii ni maji yaliyo moto sana, na usaha unaotiririka kutoka kwenye miili ya watu wa Motoni, basi na wanywe.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَءَاخَرُ مِن شَكۡلِهِۦٓ أَزۡوَٰجٌ
Na wao watakuwa na adhabu nyingine ya namna hii, aina na sampuli mbalimbali.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
هَٰذَا فَوۡجٞ مُّقۡتَحِمٞ مَّعَكُمۡ لَا مَرۡحَبَۢا بِهِمۡۚ إِنَّهُمۡ صَالُواْ ٱلنَّارِ
Na watakapoufikia Moto, hao wenye kupita vipimo katika uasi, watatukanana wao kwa wao na watasema baadhi yao kuwaambia wengine, «Hili ni kundi kubwa la watu wa Motoni ni wenye kuingia pamoja na nyinyi.» Na wao wajibu, «Hawana makaribisho mema wala nyumba zao haziwaenei ndani ya Moto. Wao ni wenye kuungulika kwa joto lake kama tunavyoungulika sisi.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
قَالُواْ بَلۡ أَنتُمۡ لَا مَرۡحَبَۢا بِكُمۡۖ أَنتُمۡ قَدَّمۡتُمُوهُ لَنَاۖ فَبِئۡسَ ٱلۡقَرَارُ
Hapo kundi la wafuasi litasema kuwaambia wale waliopita vipimo katika uasi, «Bali ni nyinyi msiokaribishwa vyema, kwa kuwa nyinyi ndio mliotusababishia makao ya Motoni kwa kule kutupoteza kwenu duniani, basi ubaya wa nyumba ya mtu kutulia ni Moto wa Jahanamu!»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
قَالُواْ رَبَّنَا مَن قَدَّمَ لَنَا هَٰذَا فَزِدۡهُ عَذَابٗا ضِعۡفٗا فِي ٱلنَّارِ
Na kundi la wafuasi liendelee kusema, «Mola wetu! Yoyote yule aliyetupoteza duniani akatuepusha na uongofu, muongezee adhabu yake Motoni maradufu.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሷድ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የስዋሂሊ ትርጉም - በዐብደላህ ሙሐመድ እና በናስር ኸሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

በዶ/ር ዐብደሏህ ሙሐመድ አቡበክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ ተተረጎመ

መዝጋት