Check out the new design

የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የስዋሂሊ ትርጉም - በዐብደላህ ሙሐመድ እና በናስር ኸሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሷድ   አንቀጽ:
وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَآءَ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا بَٰطِلٗاۚ ذَٰلِكَ ظَنُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ فَوَيۡلٞ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنَ ٱلنَّارِ
Hatukuumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yake kwa upuuzi na mchezo. Hiyo ndiyo dhana ya waliokufuru. Basi ole wao na Moto wa Siku ya Kiyama, kwa dhana yao ya ubatilifu na ukanushaji wao Mwenyezi Mungu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَمۡ نَجۡعَلُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ كَٱلۡمُفۡسِدِينَ فِي ٱلۡأَرۡضِ أَمۡ نَجۡعَلُ ٱلۡمُتَّقِينَ كَٱلۡفُجَّارِ
Je, tuwafanye walioamini wakafanya matendo mema ni kama waharibifu kwenye ardhi? Au je, tuwafanye wachamungu wenye kuamini ni kama waharibifu waliokufuru? Kusawazisha huku hakulingani na hekima ya Mwenyezi Mungu na hukumu yak, kwani hao hawalingani kwa Mwenyezi Mungu. Bali Mwenyezi Mungu Atawalipa wachamungu malipo mema na Atawatesa waharibifu walio waovu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
كِتَٰبٌ أَنزَلۡنَٰهُ إِلَيۡكَ مُبَٰرَكٞ لِّيَدَّبَّرُوٓاْ ءَايَٰتِهِۦ وَلِيَتَذَكَّرَ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ
Hiki ulicholetewa kwa njia ya wahyi, ewe Mtume, ni Kitabu tulichokuteremshia kilichobarikiwa, ili wafikirie juu ya aya zake na wazitumie njia zake za uongofu na ishara zake njema, na ili wapate kukumbuka watu wenye akili timamu yale Aliyowalazimisha Mwenyezi Mungu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَوَهَبۡنَا لِدَاوُۥدَ سُلَيۡمَٰنَۚ نِعۡمَ ٱلۡعَبۡدُ إِنَّهُۥٓ أَوَّابٌ
Na tulimtunukia Dāwūd mwanawe Sulaymān, tukamneemesha yeye (Dāwūd) kwa kumpa Sulyman, na tukamtuliza jicho lake kwake. Neema ya mja ni Sulaymān. Yeye alikuwa mwingi wa kurejea kwa Mwenyezi Mungu na kutubia Kwake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِذۡ عُرِضَ عَلَيۡهِ بِٱلۡعَشِيِّ ٱلصَّٰفِنَٰتُ ٱلۡجِيَادُ
Kumbuka pindi walipoorodheshwa mbele yake kipindi cha alasiri farasi wa asili wenye kasi za kukimbia, waliosimama kwa miguu mitatu na kuinua mguu wa nne kwa kuwa ni farasi bora na wapesi. Waliendelea kuorodheshwa mbele yake mpaka jua likachwa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَقَالَ إِنِّيٓ أَحۡبَبۡتُ حُبَّ ٱلۡخَيۡرِ عَن ذِكۡرِ رَبِّي حَتَّىٰ تَوَارَتۡ بِٱلۡحِجَابِ
Akasema, «Mimi nimehiari kupenda farasi kuliko kumtaja Mola wangu mpaka jua likachwa na macho yangu yakawa hayalioni.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
رُدُّوهَا عَلَيَّۖ فَطَفِقَ مَسۡحَۢا بِٱلسُّوقِ وَٱلۡأَعۡنَاقِ
Warudisheni hao farasi walioorodheshwa hivi punde.» Wakarudishwa, na akaingia kuipiga miguu yao na shingo zao kwa upanga kwa kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu, kwa kuwa wao walikuwa ni sababu ya Swala yake kumpita, Na ilikuwa kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kuchinja farasi yakubaliwa katika Sheria yake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَلَقَدۡ فَتَنَّا سُلَيۡمَٰنَ وَأَلۡقَيۡنَا عَلَىٰ كُرۡسِيِّهِۦ جَسَدٗا ثُمَّ أَنَابَ
Hakika tulimpa mtihani Sulaymān na tukamrushia kwenye kiti chake kipande cha mtoto aliyezaliwa katika kipindi alichoapa kuwa atawapitia wake zake na kila mmoja katika wao atamzalia shujaa atakayepigana katika njia ya Mwenyezi Mungu, na hakuseme «in shāa Allāh» (Mungu Akitaka). Akawapitia wake zake wote, na hakuna hata mmoja katika wao aliyeshika mimba isipokuwa mmoja aliyezaa mtoto nusu. Kisha Sulaymān alirudi kwa Mola Wake, akatubia
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
قَالَ رَبِّ ٱغۡفِرۡ لِي وَهَبۡ لِي مُلۡكٗا لَّا يَنۢبَغِي لِأَحَدٖ مِّنۢ بَعۡدِيٓۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡوَهَّابُ
na akasema, «Mola wangu! Nisamehe dhambi zangu na unipe ufalme mkubwa unaohusika na mimi ambao mfano wake hautakuwa kwa binadamu yoyote baada yangu. Hakika yako wewe, uliotakasika na kutukuka, ni Mwingi wa upaji na utoaji.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَسَخَّرۡنَا لَهُ ٱلرِّيحَ تَجۡرِي بِأَمۡرِهِۦ رُخَآءً حَيۡثُ أَصَابَ
Tukamkubalia maombi yake na tukamdhalilishia upepo ukawa unapita kwa amri yake ukiwa mtiifu kwake, hali ya kuwa na nguvu na kasi, ukielekea pale anapotaka,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱلشَّيَٰطِينَ كُلَّ بَنَّآءٖ وَغَوَّاصٖ
Na tukamdhalilishia Mashetani, akawa anawatumia katika kazi zake. Katika wao kulikuwa na wajenzi na wazamiaji baharini.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَءَاخَرِينَ مُقَرَّنِينَ فِي ٱلۡأَصۡفَادِ
Na wengine, nao ni waasi wa kijini, walikuwa wamefungwa pingu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
هَٰذَا عَطَآؤُنَا فَٱمۡنُنۡ أَوۡ أَمۡسِكۡ بِغَيۡرِ حِسَابٖ
Ufalme huu mkubwa na udhalilishiaji huu wa kipekee ni upaji wetu kwako, ewe Sulaymān, basi mpe unayemtaka na umnyime unayemtaka, hapana hesabu juu yako.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَإِنَّ لَهُۥ عِندَنَا لَزُلۡفَىٰ وَحُسۡنَ مَـَٔابٖ
Na hakika Sulaymān kwetu sisi, huko Akhera, atakuwa na ukaribu na marejeo mazuri.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَٱذۡكُرۡ عَبۡدَنَآ أَيُّوبَ إِذۡ نَادَىٰ رَبَّهُۥٓ أَنِّي مَسَّنِيَ ٱلشَّيۡطَٰنُ بِنُصۡبٖ وَعَذَابٍ
Mkumbuke, ewe Mtume, mja wetu Ayyūb alipomlingania Mola wake kwa kusema, «Shetani amenisababishia tabu, mashaka na maumivu katika mwili wangu, mali yangu na watu wangu!»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ٱرۡكُضۡ بِرِجۡلِكَۖ هَٰذَا مُغۡتَسَلُۢ بَارِدٞ وَشَرَابٞ
Tukamwambia, «Ipige ardhi kwa mguu wako! Yatabubujika kutoka humo maji baridi. Basi kunywa katika maji hayo na uoge, na madhara na maudhiko yatakuondokea.»
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሷድ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የስዋሂሊ ትርጉም - በዐብደላህ ሙሐመድ እና በናስር ኸሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

በዶ/ር ዐብደሏህ ሙሐመድ አቡበክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ ተተረጎመ

መዝጋት