Check out the new design

قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - قۇرئان كەرىمنىڭ ساۋاھىلچە تەرجىمىسىنى ئابدۇللا مۇھەممەد ۋە ناسىر خەمىيس تەرجىمە قىلغان. * - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى


مەنالار تەرجىمىسى سۈرە: رەھمان   ئايەت:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
هَٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِي يُكَذِّبُ بِهَا ٱلۡمُجۡرِمُونَ
Wataambiwa hao wahalifu kwa njia ya kulaumiwa na kudhalilishwa, «Huu ndio moto wa Jahanamu ambao wahalifu duniani walikuwa wakiukanusha:
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
يَطُوفُونَ بَيۡنَهَا وَبَيۡنَ حَمِيمٍ ءَانٖ
mara wanaadhibiwa kwenye Jaḥīm, na mara nyingine wananyweshwa Hāmīm, nacho ni kinywaji kilichofikia upeo wa ukali wa moto, kinakata tumbo na sehemu za ndani ya mbavu.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَلِمَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ
Na anayemcha Mwenyezi Mungu, miongoni mwa waja Wake binadamu na majini, akaogopa kusimama kwake mbele Yake, akamtii na akaacha kumuasi atakuwa na mabustani mawili ya Pepo.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
ذَوَاتَآ أَفۡنَانٖ
Mabustani mawili hayo ya Pepo yana matawi yaliyostawi kwa matunda ya kila aina.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فِيهِمَا عَيۡنَانِ تَجۡرِيَانِ
Katika Pepo mbili hizo kuna chemchemi mbili za maji zinazopita katikati yake.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فِيهِمَا مِن كُلِّ فَٰكِهَةٖ زَوۡجَانِ
Katika mabustani hayo mawili ya Pepo kuna sampuli mbili za kila aina ya matunda.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ فُرُشِۭ بَطَآئِنُهَا مِنۡ إِسۡتَبۡرَقٖۚ وَجَنَى ٱلۡجَنَّتَيۡنِ دَانٖ
Na wale wanaoogopa kusimama mbele ya Mola Wao watakuwa na mabustani mawili ya Pepo, ambayo ndani yake watastarehe, hali ya kutegemea juu ya matandiko yaliyojazwa dibaji nzito. Na matunda ya mabustani mawili hayo ya pepo yako karibu nao.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mtazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فِيهِنَّ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ لَمۡ يَطۡمِثۡهُنَّ إِنسٞ قَبۡلَهُمۡ وَلَا جَآنّٞ
Katika matandiko hayo wapo wake macho yao yanawatazama waume zao tu, hawawatazami wengineo, wamefungamana na wao. Hakuna aliyewaingilia, kabla ya hao waume zao, binadamu yoyote wala jini.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadanu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
كَأَنَّهُنَّ ٱلۡيَاقُوتُ وَٱلۡمَرۡجَانُ
Kama kwamba hawa wake wa kihurulaini ni yakuti na marijani katika sifa zao na uzuri wao.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa najini na binadamu , mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
هَلۡ جَزَآءُ ٱلۡإِحۡسَٰنِ إِلَّا ٱلۡإِحۡسَٰنُ
Je atakuwa na malipo yoyote, huyu aliyekuwa mwema wa matendo duniani, isipokuwa ni afanyiwe wema kwa kupewa Pepo huko Akhera?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ
Na chini ya mabustani ya Pepo mawili yaliyotangulia kuna mabustani ya Pepo mawili mengine.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
مُدۡهَآمَّتَانِ
Mabustani haya mawili ni rangi ya kijani. Ujani wake umeiva sana mapaka umeingia kwenye weusi.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فِيهِمَا عَيۡنَانِ نَضَّاخَتَانِ
Ndani ya mabustani mawili hayo ya Peponi kuna chemchemi mbili zenye kububujika maji daima bila kukatika.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فِيهِمَا فَٰكِهَةٞ وَنَخۡلٞ وَرُمَّانٞ
Kwenye mabustani hayo mawili kuna aina za matunda, mitende na mikomamanga.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni neema gani za Mola wenu, enyi mkusanyiko wa majini na binadamu, mnazikanusha?
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
 
مەنالار تەرجىمىسى سۈرە: رەھمان
سۈرە مۇندەرىجىسى بەت نومۇرى
 
قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - قۇرئان كەرىمنىڭ ساۋاھىلچە تەرجىمىسىنى ئابدۇللا مۇھەممەد ۋە ناسىر خەمىيس تەرجىمە قىلغان. - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

د. ئابدۇللاھ مۇھەممەد ئەبۇ بەكىر ۋە ئۇستاز ناسىر خەمىيس تەرجىمە قىلغان.

تاقاش