Check out the new design

قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - قۇرئان كەرىمنىڭ ساۋاھىلچە تەرجىمىسىنى ئابدۇللا مۇھەممەد ۋە ناسىر خەمىيس تەرجىمە قىلغان. * - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى


مەنالار تەرجىمىسى سۈرە: ئەنبىيا   ئايەت:
لَا يَسۡمَعُونَ حَسِيسَهَاۖ وَهُمۡ فِي مَا ٱشۡتَهَتۡ أَنفُسُهُمۡ خَٰلِدُونَ
Hawatasikia sauti ya mroromo wake na kuchomeka kwa miili humo, kwani wameshakaa kwenye nyumba zao huko Peponi na wamekuwa ni wenye kukaa makao ya milele katika starehe na ladha zake zinazotamaniwa na nafsi zao.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
لَا يَحۡزُنُهُمُ ٱلۡفَزَعُ ٱلۡأَكۡبَرُ وَتَتَلَقَّىٰهُمُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ هَٰذَا يَوۡمُكُمُ ٱلَّذِي كُنتُمۡ تُوعَدُونَ
Hakiwatishi wao kituko kikubwa Siku ya Kiyama, bali Malaika watawapa bishara njema kwa kuwaambia, «Hii ndiyo siku yenu mlioahidiwa maandalizi mema kutoka kwa Mwenyezi Mungu na thawabu nyingi.»
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
يَوۡمَ نَطۡوِي ٱلسَّمَآءَ كَطَيِّ ٱلسِّجِلِّ لِلۡكُتُبِۚ كَمَا بَدَأۡنَآ أَوَّلَ خَلۡقٖ نُّعِيدُهُۥۚ وَعۡدًا عَلَيۡنَآۚ إِنَّا كُنَّا فَٰعِلِينَ
Siku ambayo tutaikunja mbingu kame vile ukurasa unaokunjiwa maandishi yaliyomo ndani na tutawafufua viumbe kama vile walivyokuwa mwanzo walipozaliwa na mama zao. Hiyo ndiyo ahadi ya Mwenyezi Mungu isiyokwenda kinyume. Tumeliahidi hilo ahadi ya kweli tuliyojilazimisha nayo. Hakika sisi daima ni wenye kufanya tunaloahidi.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَلَقَدۡ كَتَبۡنَا فِي ٱلزَّبُورِ مِنۢ بَعۡدِ ٱلذِّكۡرِ أَنَّ ٱلۡأَرۡضَ يَرِثُهَا عِبَادِيَ ٱلصَّٰلِحُونَ
Na kwa hakika, tuliandika kwenye vitabu vilivyoteremshwa, baada ya kuwa yashaandikwa katika Ubao Uliohifadhiwa, kwamba ardhi watairithi waja wa Mwenyezi Mungu walio wema, wale wanaosimama imara kwa yale waliyoamrishwa na wakajiepusha na yale waliyokatazwa, nao ni ummah wa Muhammad, rehema na amani ya Mwenyezi Mungu zishukiye.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
إِنَّ فِي هَٰذَا لَبَلَٰغٗا لِّقَوۡمٍ عَٰبِدِينَ
Kwa hakika, kwenye mawaidha haya yanayosomwa pana mazingatio ya kutosha kwa watu wenye kumuabudu Mwenyezi Mungu kwa namna Aliyowaekea na Anayoiridhia kutoka kwao.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَمَآ أَرۡسَلۡنَٰكَ إِلَّا رَحۡمَةٗ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Na hatukukutumiliza , ewe Mtume, isipokuwa ni rehema kwa watu wote. Mwenye kukuamini atakuwa mwema na ataokoka, na asiyeamini atapita patupu na atapata hasara.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
قُلۡ إِنَّمَا يُوحَىٰٓ إِلَيَّ أَنَّمَآ إِلَٰهُكُمۡ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞۖ فَهَلۡ أَنتُم مُّسۡلِمُونَ
Sema, «Kile nilicholietewa wahyi na nikatumilizwa kwacho ni kwamba mola wenu Anayestahiki kuabudiwa, Peke Yake, ni Mwenyezi Mungu. Basi jisalimisheni Kwake na mnyoshe shingo zenu kwa kumuabudu.»
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَقُلۡ ءَاذَنتُكُمۡ عَلَىٰ سَوَآءٖۖ وَإِنۡ أَدۡرِيٓ أَقَرِيبٌ أَم بَعِيدٞ مَّا تُوعَدُونَ
Basi hawa wakiupuka Uislamu waambie, «Ninawafikishia nyote kile ambacho Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Amenitumia wahyi nacho. Mimi na nyinyi tuko sawa katika kuyajua yale ninayowaonya nayo na kuwatahadharisha, na mimi sijui, baada ya hapo, ni lini adhabu mliyoagiziwa itawashukia?»
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ مِنَ ٱلۡقَوۡلِ وَيَعۡلَمُ مَا تَكۡتُمُونَ
Kwa hakika Mwenyezi Mungu Anayajua mnayoyadhihirisha miongoni mwa maneno yenu na mnayoyaficha ndani ya nyoyo zenu, na Atawahesabu kwayo.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَإِنۡ أَدۡرِي لَعَلَّهُۥ فِتۡنَةٞ لَّكُمۡ وَمَتَٰعٌ إِلَىٰ حِينٖ
Na sijui huenda kukawa kule kucheleweshwa adhabu mliyoitaka iwajie kwa haraka ni mavuto na mtihani kwenu, na ili mjistareheshe ulimwenguni mpaka muda ukome, mpate kuzidisha ukafiri, kisha hiyo iwe ni sababu ya nyinyi kupata mateso makubwa zaidi.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
قَٰلَ رَبِّ ٱحۡكُم بِٱلۡحَقِّۗ وَرَبُّنَا ٱلرَّحۡمَٰنُ ٱلۡمُسۡتَعَانُ عَلَىٰ مَا تَصِفُونَ
Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, akasema,» Mola wangu! Amua baina yetu na watu wetu walioukanusha Uamuzi wa haki, na tunamuomba Mola wetu Mwingi wa rehema, tunataka msaada Wake tuzibatilishe sifa mnazombandika, enyi makafiri, za ushirikina na ukanushaji na uzushi na juu ya maonyo mnayotuonya kuwa mtakuwa na nguvu na ushindi.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
 
مەنالار تەرجىمىسى سۈرە: ئەنبىيا
سۈرە مۇندەرىجىسى بەت نومۇرى
 
قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - قۇرئان كەرىمنىڭ ساۋاھىلچە تەرجىمىسىنى ئابدۇللا مۇھەممەد ۋە ناسىر خەمىيس تەرجىمە قىلغان. - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

د. ئابدۇللاھ مۇھەممەد ئەبۇ بەكىر ۋە ئۇستاز ناسىر خەمىيس تەرجىمە قىلغان.

تاقاش