Check out the new design

വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - റുവ്വാദ് തർജമ സെൻ്റർ * - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ഖലം   ആയത്ത്:

Al-Qalam

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ
Nuun. Ninaapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.[1]
[1] Herufi hii "Nuun" na herufi nyinginezo za mkato zilizo mwanzoni mwa sura mbalimbali zinaonyesha hali ya ushindi wa Qur-ani. Kwani, washirikina walipewa changamoto kwayo, lakini wakashindwa na hawakuweza kuipinga, ilhali inajumuisha herufi hizi zinazounda lugha ya Kiarabu. Kwa hivyo, kutoweza kwa Waarabu kuleta kitu kama hicho - ingawa walikuwa ndio watu wenye ufasaha zaidi - kunaonyesha kwamba Qur-ani ni ufunuo (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyokatika.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ
Na hakika wewe una tabia tukufu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ
Karibu utaona, na wao wataona.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ
Ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ
Hakika Mola wako Mlezi ndiye ajuaye zaidi ni nani aliyeipotea njia yake, na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ
Basi usiwatii wanaokadhibisha.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ
Walitamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ
Wala usimtii kila mwingi wa kuapa, anayedharauliwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ
Mwenye kukejeli mno, anayetangatanga akieneza maneno ya kufitini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ
Mwenye kuzuia mno heri, dhalimu, mwingi wa madhambi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
Mkatili, na juu ya hayo, ni mshari aliyejipachika tu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Anaposomewa Aya zetu, husema: "(Hizi ni) simulizi za uongo za watu wa zamani!"
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ
Tutamtia alama kwenye pua yake.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ
Hakika tuliwajaribu hawa kama tulivyowajaribu wale wenye shamba, walipoapa kwamba lazima watayavuna mazao yake itakapokuwa asubuhi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ
Wala hawakusema: "Mwenyezi Mungu akipenda!"
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ
Likawa kama usiku wa giza.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ
Kisha asubuhi wakaitana.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ
Ya kwamba: "Nendeni mapema kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna."
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ
Basi walikwenda huku wananong'onezana.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ
Ya kuwa: "Leo kamwe masikini mmoja asikuingilieni."
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ
Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ
Bali tumenyimwa!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ
Basi wakaelekeana kulaumiana wao kwa wao.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ
Wakasema: Ole wetu! Hakika sisi tulikuwa tumeikiuka mipaka!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lililo bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangelijua!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Hakika wacha Mungu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَفَنَجۡعَلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ كَٱلۡمُجۡرِمِينَ
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Mna nini? Mnahukumu vipi?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ لَكُمۡ كِتَٰبٞ فِيهِ تَدۡرُسُونَ
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ لَكُمۡ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
Kuwa mtapata humo mnayoyapenda?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ لَكُمۡ أَيۡمَٰنٌ عَلَيۡنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمۡ لَمَا تَحۡكُمُونَ
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayojihukumia?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
سَلۡهُمۡ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ لَهُمۡ شُرَكَآءُ فَلۡيَأۡتُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ
Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ وَقَدۡ كَانُواْ يُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمۡ سَٰلِمُونَ
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipokuwa wazima.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَذَرۡنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِۖ سَنَسۡتَدۡرِجُهُم مِّنۡ حَيۡثُ لَا يَعۡلَمُونَ
Basi niache na wanaokadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kutokea mahali wasipopajua.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأُمۡلِي لَهُمۡۚ إِنَّ كَيۡدِي مَتِينٌ
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلۡحُوتِ إِذۡ نَادَىٰ وَهُوَ مَكۡظُومٞ
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, aliponadi naye kazongwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
لَّوۡلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعۡمَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ مَذۡمُومٞ
Kama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angelitupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱجۡتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَيُزۡلِقُونَكَ بِأَبۡصَٰرِهِمۡ لَمَّا سَمِعُواْ ٱلذِّكۡرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجۡنُونٞ
Na waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanaposikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
 
പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ഖലം
സൂറത്തുകളുടെ സൂചിക പേജ് നമ്പർ
 
വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - റുവ്വാദ് തർജമ സെൻ്റർ - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

റബ്‌വ ഇസ്‌ലാമിക് ദഅ്വാ ആൻഡ് ഗൈഡൻസ് സെൻററിൻ്റെയും കോൺടെന്റ് ഇൻ ലാംഗ്വേജസ് സർവീസ് അസോസിയേഷൻ്റെയും സഹകരണത്തോടെ മർകസ് റുവാദ് തർജമ വിഭാഗം വിവർത്തനം ചെയ്തത്.

അടക്കുക