Check out the new design

വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. * - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക


പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ന്നബഅ്   ആയത്ത്:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا
Hakika kwa wale ambao wanamuogopa Mola wao na huku wanatenda mema kuna kufaulu kwa kuingia Peponi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا
Hakika watapata Mabustani makubwa na zabibu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا
Na watapata wanawake wenye umri mdogo, wenye vifua vilivyojaza, marika na waume zao.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا
Na watapata glasi zlizojaa pombe.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّٰبٗا
Hawatasikia katika Pepo hiyo maneno ya upotofu wala kudanganyana.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا
Watayapata yote hayo yakiwa ni malipo na zawadi na kipewa kingi cha kuwatosha kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلرَّحۡمَٰنِۖ لَا يَمۡلِكُونَ مِنۡهُ خِطَابٗا
Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati ya hizo, Mwenye kuwarehemu duniani na Akhera. Hawataweza kumuomba isipokuwa kile walichopewa ruhusa kumuomba.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَوۡمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ صَفّٗاۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنۡ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَقَالَ صَوَابٗا
Siku atakaposimama Jibrili na Malaika wengine hali ya kujipanga mlolongo. Hawatamuombea isipokuwa yule aliyetolewa ruhusa na Mwingi wa Rehema ya kuombewa na akasema maneno ya haki na ya sawa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلۡحَقُّۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Hiyo ndiyo siku ya haki isiyokuwa na shaka kuja kwake. Kwa hivyo, yule atakaye kuokoka na vituko vya Siku hiyo, na ajifanyie njia ya marejeo kwa Mola wake kutenda vitendo vyema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّآ أَنذَرۡنَٰكُمۡ عَذَابٗا قَرِيبٗا يَوۡمَ يَنظُرُ ٱلۡمَرۡءُ مَا قَدَّمَتۡ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلۡكَافِرُ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ تُرَٰبَۢا
Sisi Tunawaonya nyinyi adhabu ya Siku ya mwisho iliyo karibu. Siku ambayo atayaona kila mtu aliyoyatenda katika kheri au aliyoyachuma miongoni mwa madhambi. Na kafiri atasema, kwa kitisho cha Hesabu, «Laiti mimi nilikuwa mchanga na sikufufuliwa.»
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
 
പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ന്നബഅ്
സൂറത്തുകളുടെ സൂചിക പേജ് നമ്പർ
 
വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

വിവർത്തനം: ഡോ. അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് അബൂബക്കർ & ശൈഖ് നാസ്വിർ ഖമീസ്

അടക്കുക