Check out the new design

ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಮತ್ತು ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್ * - ಅನುವಾದಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ


ಅರ್ಥಗಳ ಅನುವಾದ ಅಧ್ಯಾಯ: ಸ್ವಾದ್   ಶ್ಲೋಕ:
وَقَالُواْ مَا لَنَا لَا نَرَىٰ رِجَالٗا كُنَّا نَعُدُّهُم مِّنَ ٱلۡأَشۡرَارِ
Na watasema wale waliopita vipimo katika uasi, «Mbona hatuwaoni pamoja na sisi Motoni wale watoto ambao tulikuwa tukiwahesabu duniani kuwa ni miongoni mwa watu waovu wakorofi?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَتَّخَذۡنَٰهُمۡ سِخۡرِيًّا أَمۡ زَاغَتۡ عَنۡهُمُ ٱلۡأَبۡصَٰرُ
Je, kwani kule kuwadharau kwetu na kuwachezea kulikuwa ni makosa Au wao wako pamoja na sisi Motoni lakini macho yetu bado hayajawaona?»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِنَّ ذَٰلِكَ لَحَقّٞ تَخَاصُمُ أَهۡلِ ٱلنَّارِ
Kwa hakika, hili la kujadiliana watu wa Motoni na kuteta kwao ni jambo litakalotokea bila shaka.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قُلۡ إِنَّمَآ أَنَا۠ مُنذِرٞۖ وَمَا مِنۡ إِلَٰهٍ إِلَّا ٱللَّهُ ٱلۡوَٰحِدُ ٱلۡقَهَّارُ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia watu wako, «Hakika mimi ninawaonya nyinyi na adhabu ya Mwenyezi Mungu isiwashukie kwa sababu ya kumkanusha kwenu Mwenyezi Mungu, hakuna mola anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Yeye Peke Yake, Yeye Ndiye Aliyepwekeka kwa ukubwa Wake, majina Yake, sifa Zake na matendo Yake, Mwenye kutendesha nguvu Anayekilazimisha kila kitu na kukishinda.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡغَفَّٰرُ
Mwenye kumiliki mbingu na ardhi na vilivyoko baina yake, Aliye Mshindi katika kutesa Kwake, Mwingi wa kusamehe dhambi za aliyetubia na kurudi kutafuta radhi Zake.»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قُلۡ هُوَ نَبَؤٌاْ عَظِيمٌ
Sema, ewe Mtume kuwaambia watu wako, «Kwa hakika hii Qur’ani ni habari yenye manufaa makubwa.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَنتُمۡ عَنۡهُ مُعۡرِضُونَ
Nyinyi mmeghafilika nayo, mmejiepusha nayo na hamuitumii.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
مَا كَانَ لِيَ مِنۡ عِلۡمِۭ بِٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰٓ إِذۡ يَخۡتَصِمُونَ
«Mimi sikuwa na ujuzi wa utesi wa Malaika wa mbinguni kuhusu kuumbwa kwa Ādam, lau si Mwenyezi Mungu kunijulisha na kuniletea wahyi kwa hilo.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِن يُوحَىٰٓ إِلَيَّ إِلَّآ أَنَّمَآ أَنَا۠ نَذِيرٞ مُّبِينٌ
«Mwenyezi Mungu haniletei wahyi unaokusanya ujuzi wa kitu ambacho sina ujuzi nacho isipokuwa ni kwa kuwa mimi ni muonyaji wenu kutokana na adhabu Yake, ni mwenye kuwabainishia sheria Yake.»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَٰٓئِكَةِ إِنِّي خَٰلِقُۢ بَشَرٗا مِّن طِينٖ
Kumbuka pindi Aliposema Mola wako kuwaambia Malaika, «Hakika mimi nitamuumba kiumbe kutokana na mchanga.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَإِذَا سَوَّيۡتُهُۥ وَنَفَخۡتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُواْ لَهُۥ سَٰجِدِينَ
Basi nitakapousawazisha mwili wake na umbo lake na nikapuliza roho ndani yake na uhai ukatambaa humo, msujudieni» sijida ya heshima na kukirimu, na siyo sijida ya ibada na kutukuza. Kwani ibada haiwi isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, Peke Yake. Na Mwenyezi Mungu Ameharamisha, katika Sheria ya Kiislamu, kusujudu kwa njia ya maamkizi.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَسَجَدَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ كُلُّهُمۡ أَجۡمَعُونَ
Hapo Malaika wote wakasujudu kwa kutii na kufuata amri ya Mwenyezi Mungu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِلَّآ إِبۡلِيسَ ٱسۡتَكۡبَرَ وَكَانَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ
isipokuwa Iblisi Yeye hakusujudu kwa ujeuri na kiburi, na alikuwa, katika ujuzi wa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, ni miongoni mwa makafiri.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قَالَ يَٰٓإِبۡلِيسُ مَا مَنَعَكَ أَن تَسۡجُدَ لِمَا خَلَقۡتُ بِيَدَيَّۖ أَسۡتَكۡبَرۡتَ أَمۡ كُنتَ مِنَ ٱلۡعَالِينَ
Mwenyezi Mungu Akamwambia Iblisi, «Ni lipi lililokukataza kumsujudia yule niliyemkirimu nikamuumba kwa mikono yangu miwili? Je, umemfanyia kiburi Ādam au umekuwa ni miongoni mwa wale waliomfanyia kiburi Mola wako?» Katika aya hii pana kumthibitishia Mwenyezi Mungu, Mwenye kheri nyingi na kutukuka, sifa ya mikono miwili, kwa namna inayolingana na Yeye, kutakasika ni Kwake.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قَالَ أَنَا۠ خَيۡرٞ مِّنۡهُ خَلَقۡتَنِي مِن نَّارٖ وَخَلَقۡتَهُۥ مِن طِينٖ
Iblisi akasema akimpinga Mola wake, «Mimi sikumsujudia kwa kuwa mimi ni bora kuliko Yeye, kwa kuwa umeniumba kwa moto na umemuumba yeye kwa udongo (na moto ni bora kuliko udongo).
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قَالَ فَٱخۡرُجۡ مِنۡهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٞ
Mwenyezi Mungu Akamwambia, «Basi toka peponi! Wewe, kwa neno lako hilo, umefukuzwa, umeepushwa na kulaaniwa.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَإِنَّ عَلَيۡكَ لَعۡنَتِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلدِّينِ
Na huko kukufukuza kwangu na kukuepusha na mimi kutaendelea mpaka Siku ya Malipo na Hesabu.»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قَالَ رَبِّ فَأَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ
Iblisi akasema, «Mola wangu! ucheleweshe ukomo wa maisha yangu wala usiniangamize mpaka wakati ambapo viumbe watafufuliwa kutoka makaburini mwao».
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ
Mwenyezi Mungu Akasema kumwambia, «Wewe ni miongoni mwa watakaocheleweshwa mpaka Siku ya kipindi maalumu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ
nayo ni Siku ya Mvuvio wa Kwanza ambapo viumbe watakufa.»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قَالَ فَبِعِزَّتِكَ لَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ
Iblisi akasema, «Naapa kwa enzi yako, ewe Mola wangu, na utukufu wako! Nitawapoteza binadamu wote,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
isipokuwa wale uliowatakasa miongoni mwa waja wako na ukawalinda nisiwapoteze, na usinipatie njia yoyote ya kuwaathiri.»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
 
ಅರ್ಥಗಳ ಅನುವಾದ ಅಧ್ಯಾಯ: ಸ್ವಾದ್
ಅಧ್ಯಾಯಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ ಪುಟ ಸಂಖ್ಯೆ
 
ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಮತ್ತು ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್ - ಅನುವಾದಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ

ಅನುವಾದ - ಡಾ. ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಅಬೂಬಕರ್ ಮತ್ತು ಶೈಖ್ ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್

ಮುಚ್ಚಿ