Check out the new design

ការបកប្រែអត្ថន័យនៃគម្ពីរគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស * - មាតិកានៃការបកប្រែ


ការបកប្រែអត្ថន័យ ជំពូក​: អាល់អ៊ីមហ្វុីត័រ   វាក្យខណ្ឌ:

Al-Infitar

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ
Pindi mbingu zitakapopasuka na ukaharibika mpango wake.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ
Na pindi nyota zitakapoangukiana.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ
Na pindi Mwenyezi Mungu Atakapozifanya bahari kulipuka na maji yake kutoweka.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ
Na pindi makaburi yatakapogeuzwa kwa kufufuliwa waliokuwamo ndani yake.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ
Wakati huo itajua kila nafsi vitendo vyake vyote ilivyovifanya, vilivyotangulia na vilivyoahirika na italipwa kwa vitendo hivyo.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ
Ewe binadamu unayekanusha kufufuliwa! Ni kipi kilichokufanya uhadaike na ughurike kuhusu Mola wako Mpaji Mwenye kheri nyingi, Anayestahiki kushukuriwa na kutiiwa?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Kwani si Yeye Aliyekuumba, Akalisawazisha umbo lako, Akakuweka katika hali ya sawa na Akakurekibisha ili uweze kutekeleza nyadhifa zako,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
katika sura yoyote ile Aliyoitaka Akakuumba?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Mambo hayako kama vile mnavyosema kwamba nyinyi mna haki ya kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Hesabu na Malipo.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ
Na mjue kuwa wako na nyinyi Malaika wachunguzi,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
كِرَامٗا كَٰتِبِينَ
watukufu kwa Mwenyezi Mungu, waandishi wa yale waliyowakilishwa kuyadhibiti. Hakiwapiti, katika vitendo vyenu na siri zenu, chochote.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ
Wanayajua mnayoyafanya, ya kheri au ya shari.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ
Hakika wachamungu wanaotekeleza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa kwenye neema.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ
Hakika watu waovu waliopuuza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa katika Moto mkali.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Ukali wake, Moto huo, utawapata Siku ya Malipo.Na wala wao hawatakuwa ni wenye kughibu,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ
wakawa hawamo ndani ya Moto wa Jahanamu, si kwa kutoka wala kwa kufa.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Kisha ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ
Siku ya Hesabu, hataweza yoyote kumnufaisha yoyote. Na amri zote Siku Hiyo ni za Mwenyezi Mungu Peke yake Ambaye hakuna mwenye kumshinda, wala hakuna mwenye kumtendesha nguvu, wala hakuna mwenye kushindana na Yeye.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
 
ការបកប្រែអត្ថន័យ ជំពូក​: អាល់អ៊ីមហ្វុីត័រ
មាតិកានៃជំពូក លេខ​ទំព័រ
 
ការបកប្រែអត្ថន័យនៃគម្ពីរគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស - មាតិកានៃការបកប្រែ

ការបកប្រែដោយលោកបណ្ឌិតអាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ អាពូហ្ពើកើរ និងលោកណាសៀរ ខមុីស

បិទ