Check out the new design

ការបកប្រែអត្ថន័យនៃគម្ពីរគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស * - មាតិកានៃការបកប្រែ


ការបកប្រែអត្ថន័យ ជំពូក​: អាហ្ពាសា   វាក្យខណ្ឌ:

Abasa

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Yalidhihiri mabadiliko na mkunjiko katika uso wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
na akapa nyongo kwa sababu ya kwamba Abdallah bin Ummi Maktum alimjilia akitaka aelekezwe. Na alikuwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ameshughulika kuwalingania miamba wa Kikureshi katika Uislamu.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Ni kitu gani kinakufanya wewe ujue uhakika wa jambo lake? Kwani huenda ikawa, kwa kuuliza kwake, nafsi yake itatakasika na kusafika.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au pengine apate mazingatio zaidi na kutishika.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Basi yule alijyejitosheleza na kutouhitajia uongozi wako,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
wewe ndiye unayemjali na wapulikiza maneno yake.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na ni kitu gani kinachokupa jukumu kwako iwapo hakusafika na ukafiri wake?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama yule ambaye amekuwa na pupa la kukutana na wewe,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
na huku anamuogopa Mwenyezi Mungu asiwe na kasoro katika kupata uongofu,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
wewe unampuuza. Ilivyotakikana ufanye si kama ulivyofanya, ewe Mtume.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Hakika Sura hii ni mawaidha kwako na kwa kila anayetaka kuwaidhika.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi atakaye atamkumbuka Mwenyezi Mungu na kumtaja na atafuata Wahyi Wake.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Wahyi huu, nao ni Qur’ani, uko katika kurasa zilizotukuzwa,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
zenye kuheshimiwa, zenye cheo cha juu,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
zilizosafishwa na uchafu, uongezaji na upunguzaji.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Zilizoko mikononi mwa Malaika waandishi, mabalozi kati ya Mwenyezi Mungu na viumbe Wake, wenye maumbile mema, tabia zao ni nzuri na njema na pia matendo yao.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Amelaaniwa mtu kafiri na ataadhibiwa. Ni uovu ulioje wa ukafiri wake kwa Mola wake!
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwani hajui ni kwa kitu gani Mwenyezi Mungu Alimuumba kwacho mwanzo wake?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Mwenyezi Mungu Alimuumba kwa maji machache, nayo ni manii. Akayakadiria miongo yake.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha Akambainishia njia ya kheri na ya shari.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha humkosesha uhai, na Amemuekea mahali pa kuzikiwa.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha Akitaka Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na sifa mbaya, Atamhuisha na kumfufua baada ya kifo chake, kwa ajili ya kuhesabiwa na kulipwa.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
Mambo siyo kama yale anayoyasema kafiri na anayoyafanya. Bado hajatakeleza Aliyomuamrisha kwayo Mwenyezi Mungu katika kuamini na kutenda wema kwa kumtii.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Na azingatie binadamu, vipi Mwenyezi Mungu Amekiumba chakula chake ambacho ndicho kinachoendeleza maisha yake?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Aone kwamba Sisi Tumeyamimina maji ya mvua juu ya ardhi kwa wingi.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Kisha Tumeipasua ardhi kwa Tulivyo vitoa kutoka humo miongoni mwa mimea tofauti.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Tukaotesha humo nafaka
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
na zabibu, na nyasi za wanyama.Na mizaituni na mitende.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mabustani yenye miti mikubwa.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na matunda
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
na ndisha.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Mnajistareheshea kwazo, nyinyi na wanyama wenu.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Utakapokuja Ukelele wa Siku ya Kiyama, ambao utayatia uziwi, kwa kitisho chake, masikizi.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku mtu atakapomkimbia, kwa kitisho cha Siku Hiyo, nduguye
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
na babake na mamake na
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
mkewe na wanawe.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mmoja Siku Hiyo, atakuwa na jambo litakalomzuia asishughulike na mwingine.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Nyuso za wenye neema, Siku Hiyo, zitakuwa ni zenye kung’ara,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
zenye furaha na nderemo.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso za watu wa Motoni zitakuwa na giza,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
nyeusi, zafinikwa na unyonge.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao wenye kusifika na sifa hiyo ndiwo wale waliozikufuru neema za Mwenyezi Mungu na wakazikanusha aya zake na wakayakeuka Aliyoyaharamisha kwa kutenda maovu na kukiuka mipaka.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
 
ការបកប្រែអត្ថន័យ ជំពូក​: អាហ្ពាសា
មាតិកានៃជំពូក លេខ​ទំព័រ
 
ការបកប្រែអត្ថន័យនៃគម្ពីរគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស - មាតិកានៃការបកប្រែ

ការបកប្រែដោយលោកបណ្ឌិតអាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ អាពូហ្ពើកើរ និងលោកណាសៀរ ខមុីស

បិទ