Check out the new design

ការបកប្រែអត្ថន័យនៃគម្ពីរគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស * - មាតិកានៃការបកប្រែ


ការបកប្រែអត្ថន័យ ជំពូក​: អាស់សហ្វហ្វាត   វាក្យខណ្ឌ:
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ
Watu wa Ilyas walimkanusha Nabii wao. Basi Mwenyezi Mungu , kwa hakika, Atawakusanya Siku ya Kiyama ili wahesabiwe na wateswe.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa wale waja wa Mwenyezi Mungu waliomtakasia Mwenyezi Mungu Dini yao, basi hao ni wenye kuokoka na adhabu Yake.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Tulimfanya Ilyas awe na sifa nzuri kwa ummah waliokuja baada yake.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلۡ يَاسِينَ
Maamkizi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na sifa njema kwa Ilyas.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Na kama tulivyomlipa Ilyas malipo mema kwa utiifu wake, ndivyo tutakavyowalipa walio wema miongoni mwa waja wetu Waumini.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika yake yeye ni miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu waliomtakasia wenye kufuata amri zake kivitendo.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَإِنَّ لُوطٗا لَّمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na hakika mja wetu Lūṭ tulimchagua na tukamfanya ni miongoni mwa Mitume.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِذۡ نَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Tulipomuokoa yeye na watu wa nyumbani kwake wote,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ
isipokuwa mkongwe aliyezeeka, naye ni mke wake, ambaye aliangamia pamoja na wale walioangamia miongoni mwa watu wake kwa ukafiri wake.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawaangamiza wakanushaji waliosalia miongoni mwa watu wake.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَإِنَّكُمۡ لَتَمُرُّونَ عَلَيۡهِم مُّصۡبِحِينَ
Na hakika yenu nyinyi, enyi watu wa Makkah mnazipitia katika safari zenu nyumba za watu wa Lūṭ na athari zao katika kipindi cha asubuhi,
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَبِٱلَّيۡلِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
na pia mnazipitia katika kipindi cha usiku. Basi hamtii akilini, mkaogopa kisije kikawafika nyinyi kile kilichowafika wao?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Hakika mja wetu Yūnus, tulimchagua na tukamfanya ni miongoni mwa Mitume.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
إِذۡ أَبَقَ إِلَى ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ
Alipokimbia kutoka mji wake, akiwa na hasira juu ya watu wake, akapanda jahazi iliyojaa abiria na vyombo.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُدۡحَضِينَ
Mawimbi makubwa yakaizunguka jahazi hiyo kila upande. Na watu waliokuwa wamepanda jahazi wakapiga kura ili kupunguza shehena ili wasizame. Yūnus akawa ni miongoni mwa wale walioshindwa kwa kura.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَٱلۡتَقَمَهُ ٱلۡحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٞ
Hivyo basi akatupwa baharini na chewa akammeza, na hali ni kwamba Yūnus, amani imshukie, ameleta jambo la kumfanya alaumiwe.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَلَوۡلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلۡمُسَبِّحِينَ
Lau si yale yaliyotangulia kwake, ya wingi wa Ibada na matendo mema kabla ya kuingia ndani ya tumbo la chewa kwa kusema, «Hapana Mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe, kutakasika na sifa za upungufu ni kwako, mimi nimekuwa miongoni mwa wenye kudhulumu,»
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
لَلَبِثَ فِي بَطۡنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ
angalikaa ndani ya tumbo la chewa, na lingalikuwa ni kaburi lake mpaka Siku ya Kiyama.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
۞ فَنَبَذۡنَٰهُ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٞ
Tukamtoa kwenye tumbo la chewa na tukamtupa kwenye ardhi tupu, isiyokuwa na miti wala majengo, akiwa dhaifu wa mwili.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَأَنۢبَتۡنَا عَلَيۡهِ شَجَرَةٗ مِّن يَقۡطِينٖ
Na tukamuoteshea mmea wa matango ili umfinike na anufaike nao.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَأَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ مِاْئَةِ أَلۡفٍ أَوۡ يَزِيدُونَ
Tukamtumiliza aende kwa watu wake wanaofikia elfu mia moja, bali wanazidi idadi hiyo.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَـَٔامَنُواْ فَمَتَّعۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ حِينٖ
Wakamuamini na wakafuata aliyokuja nayo kivitendo, na kwa hivyo tukawastarehesha maishani mwao mpaka wakati wa kufika ajali zao.
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَلِرَبِّكَ ٱلۡبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلۡبَنُونَ
Basi waulize watu wako, ewe Mtume, «Ni vipi wamemfanya Mwenyezi Mungu ana watoto wa kike ambao wao wenyewe wanawachukia, na wao wana watoto wa kiume wanaowataka?»
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
أَمۡ خَلَقۡنَا ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ إِنَٰثٗا وَهُمۡ شَٰهِدُونَ
Na waulize wao, «Je, tuliwaumba Malaika wakiwa wanawake, na hali wao wapo (wakishuhudia uumbaji huo)?»
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
أَلَآ إِنَّهُم مِّنۡ إِفۡكِهِمۡ لَيَقُولُونَ
Na miongoni mwa urongo wao ni kule kusema kwao, «Mwenyezi Mungu Amezaa!
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ
Na kwa hakika, wao ni warongo, kwa kuwa wanakisema wasichokijua.»
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
أَصۡطَفَى ٱلۡبَنَاتِ عَلَى ٱلۡبَنِينَ
Ni kwa kitu gani Mwenyezi Mungu Achague watoto wa kike na sio wa kiume?
ការបកស្រាយជាភាសា​អារ៉ាប់:
 
ការបកប្រែអត្ថន័យ ជំពូក​: អាស់សហ្វហ្វាត
មាតិកានៃជំពូក លេខ​ទំព័រ
 
ការបកប្រែអត្ថន័យនៃគម្ពីរគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស - មាតិកានៃការបកប្រែ

ការបកប្រែដោយលោកបណ្ឌិតអាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ អាពូហ្ពើកើរ និងលោកណាសៀរ ខមុីស

បិទ